KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA KĨA 30
RWĨMBO 97 Uhai Unategemea Neno la Mungu
Rĩ, no Wiritane Kuumania na Mooritani ja Mũsingi ja Bibiria?
“Kinya bukeethirwa ibwiji mantu jau, na ningi buriki mantune ja mma jaria bukeethirwa buri najo, uni no nkeethagirwa magiita jonthe mpendete kuburiikania jo.”—2 PET. 1:12.
JAMBO KUU
Jinsi ya kutumia masomo muhimu yanayotokana na mafundisho ya msingi ya Biblia hata miaka mingi baada ya kujifunza mambo hayo.
1. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ mooritani ja Bibiria jaakũringithĩrie ũrĩkwambia kwiritana ũmma?
MAFUNDISHO ya msingi ya Biblia yamebadili maisha yetu. Kwa mfano, tulipojifunza kwamba jina la Mungu ni Yehova, tulichukua hatua ya kwanza kuwa rafiki yake. (Isa. 42:8) Tulipojifunza ukweli kuhusu hali ya wafu, hatukuendelea kuwaza ikiwa wapendwa wetu waliokufa wanateseka. (Mhu. 9:10) Na tulipojifunza kuhusu ahadi ya Mungu ya dunia Paradiso, hatukuendelea kuwa na wasiwasi kuhusu wakati wetu ujao. Tukawa na uhakika kwamba tutaishi, si tu kwa muda mfupi, yaani, miaka 70 au 80, bali milele.—Zab. 37:29; 90:10.
2. Nĩ na njĩra ĩrĩkũ 2 Petero 1:12, 13 ĩkwonania atĩ kinya Akristũ baagimaru gĩkĩrundu nĩbagunĩkaga kuumania na mooritani ja mũsingi ja Bibiria?
2 Hatupaswi kamwe kuchukulia kivivi hivi mafundisho ya msingi ya Biblia. Katika barua yake ya pili, mtume Petro aliwaandikia Wakristo waliokuwa “imara katika kweli.” (Soma 2 Petro 1:12, 13.) Hata hivyo, walikabili hatari za kiroho katika kutaniko, kutia ndani walimu wa uwongo na watu wasiomwogopa Mungu. (2 Pet. 2:1-3) Petro alitaka kuwaimarisha ndugu na dada zake ili kuwasaidia wajilinde dhidi ya hatari hizo. Hivyo, aliwakumbusha baadhi ya mafundisho ambayo tayari walikuwa wamejifunza. Mafundisho hayo yangewasaidia kudumisha utimilifu wao hadi mwisho.
3. Taarĩĩria nĩkĩ Akristũ bonthe babuĩrĩte gwĩta na mbere kũthũgaanĩria mooritani ja mũsingi ja Bibiria.
3 Hata ikiwa sisi ni Wakristo wakomavu, bado tunaweza kujifunza mambo mapya kutokana na mafundisho ya msingi ya Biblia. Fikiria mfano huu: Mpishi stadi na mpishi mwingine ambaye bado anajifunza, wanaweza kutumia viungo vilevile vya msingi wanapotayarisha mlo fulani. Lakini baada ya muda, yule mpishi mwenye uzoefu amejifunza kutumia vizuri viungo hivyo kwa njia nyingi mbalimbali ili kutayarisha vyakula vipya vitamu. Vivyo hivyo, huenda wale ambao wamemtumikia Yehova kwa muda mrefu wakajifunza mambo mengi zaidi katika andiko fulani kuliko wale ambao wameanza kujifunza Biblia. Huenda hali zetu au mapendeleo ya utumishi yamebadilika tangu tulipobatizwa. Tunapotafakari kuhusu mafundisho ya Biblia tuliyojifunza zamani, tutatambua njia mpya tunazoweza kutumia mambo hayo katika hali tunazokabili sasa. Acheni tuone mambo ambayo Wakristo wakomavu wanaweza kujifunza kutokana na mafundisho matatu ya msingi ya Biblia.
JEHOVA NĨWE ŨŨMBĨTE INTO BIONTHE
4. Kwiritana atĩ Jehova nĩwe ũũmbĩte into bionthe kwĩthĩrĩtwe na maumĩĩra jarĩkũ ũtũũrone bwetũ?
4 “Yule aliyevijenga vitu vyote ni Mungu.” (Ebr. 3:4) Tunajua kwamba sayari yetu na viumbe vyote vilivyo ndani yake vimeumbwa na Muumba mwenye hekima na nguvu zote. Ametuumba, hivyo anatujua vizuri sana. Zaidi ya hilo, anatujali. Anajua mambo yanayotufaa zaidi. Kujua kweli hiyo rahisi, kwamba Yehova ndiye Muumba, kumekuwa na matokeo makubwa sana kwetu na kutupatia kusudi la kweli maishani.
5. Nĩ ũmma bũrĩkũ bwa Bibiria bũũmba gũtũtethia gũkũria nkuma ya winyiia? (Isaya 45:9-12)
5 Ukweli wa kwamba Yehova ndiye Muumba unaweza kutufundisha kuwa wanyenyekevu. Baada ya Ayubu kujikazia uangalifu kupita kiasi na kuwakazia fikira watu wengine, Yehova alimkumbusha kwamba Yeye ndiye Muumba Mweza-Yote. (Ayu. 38:1-4) Kikumbusho hicho kilimsaidia Ayubu kuona kwamba njia za Mungu ni kuu kuliko njia za mwanadamu. Kupatana na hilo, baadaye nabii Isaya aliandika hivi: “Je, udongo unapaswa kumuuliza Mfinyanzi: ‘Unatengeneza nini?’”—Soma Isaya 45:9-12.
6. Nĩ ĩgiita rĩrĩkũ tũkũbatara kũthũgaanĩria inya ya Jehova arĩ mũũmbi weetũ? (Tega kinya mbica.)
6 Kadiri Mkristo anavyopata uzoefu, anaweza kuanza kutumaini kupita kiasi maoni yake mwenyewe badala ya kutafuta mwongozo kutoka kwa Yehova na Neno Lake. (Ayu. 37:23, 24) Lakini namna gani ikiwa mtu atafikiria kwa kina kuhusu hekima na ukuu usio na kifani wa Muumba wake? (Isa. 40:22; 55:8, 9) Kweli hiyo ya msingi itamsaidia kuendelea kuwa mnyenyekevu na kutambua kwamba maoni ya Yehova ndiyo ya muhimu zaidi.
Ni jambo gani linaloweza kutusaidia kudumisha mtazamo unaofaa kuhusu maoni yetu? (Tazama fungu la 6)d
7. Nĩmbi Rahela aathithĩrie nĩkenda etĩkĩĩria ũgarũrũku bwa ũthuranĩri bwa Jehova?
7 Rahela, anayeishi nchini Slovenia, ametambua kwamba kufikiria kumhusu Muumba wake kumemsaidia kukubali mabadiliko ya kitengenezo. Anakiri hivi: “Nyakati fulani, haijawa rahisi kwangu kukubali maamuzi yaliyofanywa na wale wanaoongoza. Kwa mfano, hata baada ya kutazama Ripoti ya 8 ya Baraza Linaloongoza ya 2023, nilishangaa nilipomwona kwa mara ya kwanza ndugu aliyefuga ndevu akitoa hotuba. Hivyo, nilimwomba Yehova anisaidie kukubali badiliko hilo.” Rahela alitambua kwamba Yehova akiwa Muumba wa mbingu na dunia, anaweza kabisa kuliongoza tengenezo lake kwa njia inayofaa. Ikiwa ni vigumu kwako kukubali uelewaji mpya au mwongozo mpya, kwa nini usitafakari kwa unyenyekevu kuhusu hekima na nguvu zilizo kuu za Muumba wetu?—Rom. 11:33-36.
NĨKĨ MŨRUNGU ETĨKĨRĨĨTIE MĨTHANGĨKO?
8. Nĩatĩa ũgunĩkĩte kuumania na kwiritana nĩkĩ Mũrungu etĩkĩĩrĩtie mĩthangĩko?
8 Kwa nini Mungu anaruhusu kuteseka? Baadhi ya watu ambao wameshindwa kujibu swali hilo wamemkasirikia Mungu au wamefikia mkataa kwamba hakuna Mungu! (Met. 19:3) Tofauti na hilo, umejifunza kwamba kuteseka kunasababishwa na dhambi tuliyorithi na kukosa ukamilifu, na si Yehova. Pia, umejifunza kwamba subira ya Yehova kwa wanadamu imewawezesha mamilioni ya watu kumjua na kujionea wenyewe jinsi Yehova atakavyoondoa kabisa kuteseka. (2 Pet. 3:9, 15) Kweli hizo zimekufariji na kukusaidia umkaribie zaidi.
9.Nĩ magiita jarĩkũ tũbataraga kũriikana nĩkĩ Jehova etĩkĩĩrĩtie mĩthangĩko?
9 Tunaelewa umuhimu wa kuwa na subira tunapoendelea kumngojea Yehova aondoe kuteseka. Hata hivyo, sisi au wapendwa wetu wanapokabili taabu, ukosefu wa haki, au kufiwa, huenda tukajiuliza kwa nini Yehova hachukui hatua haraka zaidi. (Hab. 1:2, 3) Katika pindi hizo, litakuwa jambo la hekima kutafakari kwa nini Yehova anaruhusu waadilifu wakabili matatizo.a (Zab. 34:19) Tunaweza pia kutafakari kuhusu kusudi la Yehova la kuondoa kabisa kuteseka.
10. Nĩmbi bitethetie Anne kũũmbana na kĩeba kĩa gũkuĩrwa nĩ ngʼina?
10 Kujua ukweli kuhusu kuteseka kunaweza kutusaidia kuvumilia. Anne, anayeishi kwenye kisiwa cha Mayotte, katika Bahari ya Hindi, anasema hivi: “Nilihuzunika sana mama yangu alipokufa miaka michache iliyopita. Hata hivyo, mara kwa mara mimi hujikumbusha kwamba Yehova hasababishi kuteseka. Anatazamia kwa hamu kuondoa kila aina ya kuteseka na kuwafufua wapendwa wetu. Kutafakari kuhusu kweli hizo hunipatia amani ya akili ambayo mara nyingi hunishangaza.”
11. Kũmenya itũmi bia Jehova bia gwĩtĩkĩĩria mĩthangĩko ĩthĩrwa ĩrĩo gũtũtethagia atĩa gwĩta na mbere gũtũmĩĩria?
11 Kujua ukweli kuhusu kwa nini Mungu ameruhusu kuteseka kunaweza kutuchochea kuendelea kuhubiri. Baada ya kufafanua kwamba subira ya Yehova inamaanisha wokovu kwa wale wanaotubu, Petro aliandika hivi: “Fikirieni mnapaswa kuwa watu wa aina gani katika matendo matakatifu ya mwenendo na vitendo vya ujitoaji-kimungu.” (2 Pet. 3:11) “Vitendo vya ujitoaji-kimungu” vinatia ndani utumishi wa shambani. Kama Baba yetu, sisi pia tunawapenda watu. Tunataka waishi katika ulimwengu mpya wa Mungu wenye uadilifu. Kwa subira, Yehova anawapatia watu katika eneo lenu nafasi ya kumwabudu. Ni pendeleo kubwa sana kuwa mfanyakazi mwenzi wa Mungu na kuwasaidia wengi kadiri iwezekanavyo wajifunze kumhusu kabla ya mwisho kufika!—1 Kor. 3:9.
TŨRĨTŨŨRA ‘NTUKŨNE CIA MŨTHIAʼ
12. Nĩatĩa kwiritana atĩ tũrĩtũũra ‘ntukũne cia mũthiaʼ gũtũgunĩte?
12 Biblia inafafanua kwa usahihi watu wangekuwaje katika “siku za mwisho.” (2 Tim. 3:1-5) Tunajionea utimizo wa unabii huo tunapotazama tabia za watu wanaotuzunguka. Tunapoona mitazamo ya watu ikizidi kuwa mibaya, tunasadiki hata zaidi kwamba Neno la Mungu linategemeka.—2 Tim. 3:13-15.
13. Nĩ biũria birĩkũ tũũmba gũciũria kuumania na ngerekano ya Jesũ ĩrĩa ĩrĩ kĩrĩ Luka 12:15-21?
13 Kujua kwamba tunaishi katika siku za mwisho kunatusaidia kuwa na hisi ya uharaka. Ona jambo tunaloweza kujifunza kuhusu hisi ya uharaka katika mfano wa Yesu unaopatikana kwenye Luka 12:15-21. (Soma.) Kwa nini mwanamume huyo tajiri aliitwa “mpumbavu”? Si kwa sababu mwanamume huyo alikuwa tajiri, bali kwa sababu alitanguliza maishani mambo yasiyofaa. Alijiwekea “hazina lakini [hakuwa] tajiri kwa Mungu.” Kwa nini alihitaji kuchukua hatua haraka? Mungu alimwambia mwanamume huyo hivi: “Usiku huu wanautaka uhai wako.” Leo, kadiri mwisho wa mfumo huu wa mambo unavyokaribia, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Je, malengo yangu maishani yanaonyesha kwamba nina hisi ya uharaka? Namna gani kuhusu malengo ambayo ninawasaidia watoto wangu wajiwekee? Je, ninatumia nguvu, wakati, na pesa zangu kwa ajili yangu mwenyewe au kwa ajili ya kujiwekea hazina mbinguni?’
14. Kũringana na ngerekano ya Miki, nĩkĩ bũrĩ ũntũ bwa ũũme kwirikithĩria kuuma maandĩkone atĩ tũrĩtũũra ntukũne cia mũthia?
14 Mtazamo wetu maishani unaweza kubadilika kabisa tunapofikiria kuhusu uthibitisho wa kwamba tunaishi katika siku za mwisho. Jambo hilo lilitokea kwa dada anayeitwa Miki. Anaeleza hivi: “Nilipohitimu shule ya sekondari, nilitamani sana kwenda chuo kikuu ili kujifunza kuhusu wanyama. Pia, nilikuwa na lengo la kuwa painia wa kawaida na kutumikia katika eneo lenye uhitaji mkubwa. Marafiki wangu wakomavu walinishauri nitafakari kwa makini ikiwa ningeweza kufuatilia kazi niliyotaka na wakati uleule nitimize malengo yangu ya kiroho. Walinikumbusha kwamba karibuni mfumo huu wa mambo utafikia mwisho wake. Kwa upande mwingine, katika ulimwengu mpya, nitajifunza kuhusu wanyama wengi kadiri ninavyopenda kwa umilele wote. Hivyo, nikachagua masomo ambayo hayakuchukua muda mrefu na yaliyonisaidia kupata ustadi hususa. Hilo lilinisaidia kupata kazi iliyonitegemeza katika upainia wa kawaida na baadaye nilipohamia Ekuado, katika eneo lenye uhitaji mkubwa.” Sasa Miki na mume wake wanatumikia katika kazi ya kuzungukia makutaniko katika nchi hiyo.
15. Nĩkĩ tũtĩbuĩrĩte kuunĩka nkoro kinya rĩrĩa antũ bamwe barega gwĩtĩkĩĩria nkuma ĩnjega? Eejana ngerekano. (Tega kinya mbica)
15 Hatupaswi kuvunjika moyo watu wanapokataa habari njema mwanzoni. Watu wanaweza kubadilika. Fikiria mfano wa Yakobo, ndugu nusu ya Yesu. Alimwona Yesu akikua, akiwa Masihi, na kufundisha kwa njia bora kuliko mwanadamu yeyote mwingine. Hata hivyo, kwa miaka mingi Yakobo hakumfuata Yesu. Ni baada tu ya Yesu kufufuliwa ndipo alipokuwa mwanafunzi—isitoshe mwenye bidii sana!b (Yoh. 7:5; Gal. 2:9) Ni jambo la muhimu kutokata tamaa inapohusu watu wako wa ukoo ambao bado hawajaonyesha wanapendezwa na kweli au inapohusu kuwatembelea tena wale ambao hawakukubali ujumbe wa Ufalme. Kumbuka kwamba tunaishi katika siku za mwisho, hivyo kazi yetu ya kuhubiri ni yenye uharaka. Mambo utakayowaambia watu leo huenda yakawasaidia baadaye, huenda hata baada ya dhiki kuu.c
Ni nini kinachoweza kutuchochea kutokata tamaa inapohusu watu wetu wa ukoo wasio waamini? (Tazama fungu la 15)e
ĨTA NA MBERE KWONANIA NKAATHO TONTŨ BWA IRIKANIA BIA JEHOVA
16. Nĩatĩa ũgunĩkĩte kuumania na irikania bia Jehova? (Tega kinya kathandũkũ “Tumia Habari Hizi Kuwasaidia Wengine.”)
16 Baadhi ya chakula cha kiroho tunachopata kimeandaliwa kwa ajili ya watu ambao hawajawahi kusikia kweli za msingi za Biblia. Kwa mfano, hotuba ya watu wote inayotolewa kila juma, baadhi ya makala na video zinazopatikana katika jw.org, na magazeti yetu kwa ajili ya watu wote yameandaliwa kihususa kwa ajili ya watu ambao si Mashahidi. Ingawa hivyo, tunanufaika kutokana na vikumbusho hivyo. Vinaimarisha upendo wetu kwa Yehova, imani yetu katika Neno lake, na kutusaidia kuwafundisha wengine kweli za msingi kwa njia yenye matokeo zaidi.—Zab. 19:7.
17. Nĩ magiita jarĩkũ ũkũbatara kũriikana mooritani ja mũsingi ja Bibiria?
17 Tukiwa Mashahidi wa Yehova, tunafurahi sana wakati uelewaji wetu wa kweli fulani ya Kimaandiko unaporekebishwa. Hata hivyo, tunathamini sana pia mafundisho ya msingi ya Biblia ambayo mwanzoni yalituvuta katika kweli. Ikiwa tutashawishika kusisitiza maoni yetu badala ya kutii mwongozo kutoka katika tengenezo la Yehova, kwa unyenyekevu tunaweza kukumbuka kwamba Muumba mwenye hekima na nguvu zote, ndiye anayeongoza tengenezo hili. Sisi au mpendwa wetu anapovumilia jaribu, tunaweza kuwa na subira na kutafakari kwa nini Yehova ameruhusu kuteseka. Na tunapoamua jinsi ya kutumia wakati na mali zetu, tunaweza kukumbuka kwamba tunaishi katika siku za mwisho, na hivyo tunahitaji kuwa na hisi ya uharaka. Acheni vikumbusho vya Yehova viendelee kutuimarisha, kutuchochea, na kutupatia hekima.
RWĨMBO 95 Nuru Inazidi Kuongezeka
a Tazama makala, “Sababu Kwa Nini Mateso Yote Yatakwisha Karibuni” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 15, 2007, uku. 21-25.
c Tazama makala “Tunajua Nini Kuhusu Hukumu za Yehova za Wakati Ujao?” katika gazeti la Mnara wa Mlinzi la Mei 2024, uku. 8-13.
d MAELEZO YA PICHA: Pendekezo la mzee halijakubaliwa na baraza la wazee. Baadaye, akiwa chini ya anga lenye nyota nyingi, anachochewa kuwa na mtazamo unaofaa kuhusu maoni yake.
e MAELEZO YA PICHA: Wakati wa funzo lake la kibinafsi, dada Mkristo anachunguza ushahidi kwamba tunaishi katika siku za mwisho. Jambo hilo linamchochea kumpigia simu dada yake wa kimwili na kumhubiria.