Ayubu
29 Naye Ayubu akatokeza tena neno lake la kimethali, akaendelea kusema:
2 “Laiti ningekuwa kama nilivyokuwa katika miezi ya zamani,+
Kama katika siku ambazo Mungu alikuwa akinilinda;+
4 Kama nilivyokuwa katika siku zilizo bora za ujana wangu,+
Wakati urafiki wa karibu pamoja na Mungu ulikuwa katika hema langu;+
5 Wakati Mweza-Yote alipokuwa bado pamoja nami,
Wakati watumishi wangu walipokuwa wamenizunguka pande zote!
7 Nilipoenda kwenye lango lililo karibu na mji,+
Nilikuwa nikitayarisha kiti changu katika kiwanja cha watu wote!+
11 Kwa maana sikio lilisikiliza, likanitangaza kuwa mwenye furaha,
Nalo jicho liliona, likanishuhudia.
12 Kwa maana nilikuwa nikimwokoa mwenye kuteseka anayelia apewe msaada,+
Na mvulana asiye na baba na mtu yeyote ambaye hakuwa na msaidizi.+
13 Baraka+ ya mtu aliye karibu kuangamia—ilikuwa ikija juu yangu,
Na moyo wa mjane nilikuwa nikiufurahisha.+
14 Nilivaa uadilifu, nao ulikuwa ukinivika.+
Haki yangu ilikuwa kama koti lisilo na mikono—na kilemba.
17 Nami nilikuwa nikiivunja mifupa ya taya ya mkosaji,+
Na kutoka katika meno yake nikawa nikinyakua mawindo.
18 Na nilikuwa nikisema, ‘Nitakata pumzi+ ndani ya kiota changu,
Nami nitazidisha siku zangu kama chembe za mchanga.+
20 Utukufu wangu ni mpya kwangu,
Na upinde wangu mkononi mwangu utapiga tena na tena.’