Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 18:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Nao wakawahukumu watu katika kila pindi inayofaa. Kesi ngumu walikuwa wakimletea Musa,+ lakini kila kesi ndogo wao wenyewe waliishughulikia wakiwa waamuzi.

  • Kumbukumbu la Torati 16:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 “Utaweka waamuzi+ na maofisa+ kwa ajili yako ndani ya malango yote ambayo Yehova Mungu wako anakupa wewe kulingana na makabila yako, nao watawahukumu watu kwa hukumu ya uadilifu.

  • Kumbukumbu la Torati 17:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 “Ikiwa jambo la uamuzi wa hukumu litakuwa lisilo la kawaida kwako,+ ambamo damu imemwagwa,+ ambamo dai halali limezushwa,+ au tendo lenye jeuri limefanywa, mambo ya mzozo,+ ndani ya malango yako, utaondoka pia na kwenda mahali ambapo Yehova Mungu wako atapachagua,+

  • Kumbukumbu la Torati 22:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Nao wanaume wazee+ wa jiji hilo watamchukua mwanamume huyo na kumtia nidhamu.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 19:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Na kuhusu kila kesi itakayokuja kwenu ya ndugu zenu wanaokaa katika majiji yao, inayohusu kumwaga damu,+ inayohusu sheria+ na amri+ na masharti+ na maamuzi ya hukumu,+ lazima mwaonye kwamba wasimkosee Yehova ili ghadhabu+ isije juu yenu na juu ya ndugu zenu. Hivyo ndivyo mnavyopaswa kufanya ili msipate hatia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki