Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 13:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Ndipo akaipaazia sauti ile madhabahu kwa neno la Yehova, akasema: “Ee madhabahu, madhabahu, Yehova amesema hivi, ‘Tazama! Mwana aliyezaliwa katika nyumba ya Daudi, ambaye jina lake ni Yosia!+ Naye atawatoa juu yako wawe dhabihu wale makuhani wa mahali pa juu wanaofukiza moshi wa dhabihu juu yako, naye atateketeza mifupa ya watu juu yako.’”+

  • 2 Wafalme 23:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Kisha akaleta makuhani wote kutoka katika majiji ya Yuda, ili apafanye pasifae kwa ibada mahali pa juu ambapo makuhani walifukiza moshi wa dhabihu, kuanzia Geba+ mpaka Beer-sheba;+ naye akabomoa mahali pa juu pa malango yaliyokuwa katika mwingilio wa lango la Yoshua, mkuu wa jiji, ambapo palikuwa upande wa kushoto mtu anapoingia katika lango la jiji.

  • 2 Mambo ya Nyakati 34:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Na katika mwaka wa nane wa kutawala kwake, alipokuwa angali mvulana,+ akaanza kumtafuta+ Mungu wa Daudi babu yake; na katika mwaka wa kumi na mbili akaanza kutakasa+ Yuda na Yerusalemu kutokana na mahali pa juu+ na miti mitakatifu+ na sanamu za kuchongwa+ na sanamu za kuyeyushwa.

  • Isaya 27:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Basi kwa njia hii kosa la Yakobo litafanyiwa upatanisho,+ na haya ni matunda yote wakati anapoiondoa dhambi yake,+ wakati anapofanya mawe yote ya madhabahu kama mawe ya chokaa ambayo yamepondwa, hivi kwamba miti mitakatifu+ na vinara vya uvumba havitasimama.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki