18 “Roho ya Yehova+ iko juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuwatangazia maskini habari njema, alinituma kuhubiri kuachiliwa huru kwa mateka na kupata kuona tena kwa vipofu, kuacha waliopondeka waende zao wakiwa wameachiliwa huru,+
38 yaani, Yesu aliyekuwa ametoka Nazareti, jinsi Mungu alivyomtia mafuta kwa roho takatifu+ na nguvu, naye akaenda akipita katika nchi akitenda mema na kuwaponya wote waliokandamizwa na Ibilisi;+ kwa sababu Mungu alikuwa pamoja naye.+
5Kwa maana kila kuhani mkuu anayechukuliwa kutoka kati ya wanadamu huwekwa rasmi kwa ajili ya wanadamu juu ya mambo yanayohusiana na Mungu,+ ili atoe zawadi na dhabihu kwa ajili ya dhambi.+
28 kwa maana Sheria huweka rasmi kuwa makuhani wakuu+ watu walio na udhaifu,+ lakini neno la kiapo+ rasmi lililokuja baada ya Sheria humweka rasmi Mwana, ambaye amekamilishwa+ milele.