5 Na sasa ikiwa mtaitii+ sauti yangu kabisa na kulishika kwa kweli agano+ langu, ndipo hakika mtakapokuwa mali yangu ya pekee kutoka kati ya vikundi vingine vyote vya watu,+ kwa sababu dunia nzima ni yangu.+
16 Na sasa itajulikana jinsi gani kwamba nimepata kibali machoni pako, mimi na watu wako? Je, si kwa wewe kwenda pamoja nasi,+ kwa kuwa mimi na watu wako tumefanywa tofauti na watu wengine wote walio juu ya uso wa nchi?”+
53 Kwa maana wewe mwenyewe uliwatenga wawe urithi wako kutoka katika vikundi vyote vya watu wa dunia,+ kama vile ulivyosema kupitia mtumishi wako Musa+ ulipokuwa ukiwatoa mababu zetu kutoka Misri, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.”
16 Na hekalu la Mungu lina upatano gani na sanamu?+ Kwa maana sisi ni hekalu+ la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema: “Mimi nitakaa katikati yao+ na kutembea katikati yao, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”+
9 Lakini ninyi ni “jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu,+ watu wa kuwa mali ya pekee,+ ili mtangaze kotekote sifa bora”+ zake yeye aliyewaita ninyi kutoka katika giza kuingia katika nuru yake ya ajabu.+