18 Nao Mlima Sinai ukatoa moshi kila mahali,+ kwa kuwa Yehova alikuwa ameshuka juu yake katika moto;+ na moshi wake ukawa ukipaa kama moshi wa tanuru,+ na mlima wote ulikuwa ukitetemeka sana.+
11 “Kwa hiyo mkaja karibu na kusimama chini ya mlima, nao mlima ulikuwa ukiwaka moto mpaka katikati ya mbingu; kulikuwa na giza, wingu na weusi mzito.+