Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 15:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Hata hivyo, mtu yeyote asije kuwa maskini katikati yako, kwa sababu hakika Yehova atakubariki+ katika nchi ambayo Yehova Mungu wako anakupa iwe urithi, uimiliki,+

  • Kumbukumbu la Torati 24:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 “Ikiwa utavuna mavuno ya shamba lako,+ nawe umesahau mganda shambani, hupaswi kurudi kuuchukua. Huo utakaa kwa ajili ya mkaaji mgeni, kwa ajili ya mvulana asiye na baba na kwa ajili ya mjane;+ ili Yehova Mungu wako akubariki katika kila tendo la mkono wako.+

  • Zaburi 41:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 41 Mwenye furaha ni mtu yeyote anayetenda kwa kumfikiria mtu wa hali ya chini;+

      Katika siku ya msiba Yehova atamwokoa.+

  • Methali 22:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa, kwa maana amempa mtu wa hali ya chini chakula chake.+

  • Isaya 32:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Naye mtu mkarimu, ametoa shauri kwa ajili ya mambo ya ukarimu; naye atasimama kwa ajili ya mambo ya ukarimu.+

  • 2 Wakorintho 9:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Zaidi ya hayo, Mungu anaweza kufanya fadhili zake zote zisizostahiliwa ziwe nyingi kuwaelekea ninyi, ili, ijapokuwa sikuzote mna ujitoshelevu kamili katika kila kitu, muwe na vingi kwa ajili ya kila kazi njema.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki