13 Naye akaanza kumwambia Abramu: “Ujue hakika kwamba uzao wako utakuwa mkaaji mgeni katika nchi isiyokuwa yao,+ nao watawatumikia watu wale, nao watawatesa kwa miaka mia nne.+
7 Naye Yehova akaongezea: “Pasipo shaka nimeyaona mateso ya watu wangu walio Misri, nami nimesikia kilio chao kwa sababu ya wale wanaowalazimisha kufanya kazi; kwa sababu nayajua vizuri maumivu waliyo nayo.+
15 Nawe ukumbuke kwamba ulikuwa mtumwa katika nchi ya Misri+ na Yehova Mungu wako akakutoa huko kwa mkono wenye nguvu na kwa mkono ulionyooshwa.+ Ndiyo sababu Yehova Mungu wako alikuamuru uendelee kuishika siku ya sabato.+