Waamuzi 19:30 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 30 Na ikatukia kwamba kila mtu aliyeona jambo hilo akasema: “Jambo kama hili halijawahi kutokea kamwe wala kuonekana tangu siku wana wa Israeli walipopanda kutoka nchi ya Misri mpaka leo. Wekeni jambo hili mioyoni mwenu, fanyeni shauri+ na mseme.” Methali 11:14 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 14 Wakati ambapo hakuna mwongozo stadi, watu huanguka;+ lakini kwa wingi wa washauri kuna wokovu.+ Methali 13:10 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 10 Kwa sababu ya kimbelembele mtu husababisha tu pambano,+ lakini wale wanaoshauriana pamoja wana hekima.+ Methali 20:18 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 18 Kwa shauri mipango yenyewe hufanywa imara,+ na kwa mwongozo stadi endeleza vita vyako.+ Methali 24:6 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 6 Kwa maana kwa mwongozo stadi utaendeleza vita vyako,+ na kwa wingi wa washauri kuna wokovu.+
30 Na ikatukia kwamba kila mtu aliyeona jambo hilo akasema: “Jambo kama hili halijawahi kutokea kamwe wala kuonekana tangu siku wana wa Israeli walipopanda kutoka nchi ya Misri mpaka leo. Wekeni jambo hili mioyoni mwenu, fanyeni shauri+ na mseme.”
10 Kwa sababu ya kimbelembele mtu husababisha tu pambano,+ lakini wale wanaoshauriana pamoja wana hekima.+