Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 9:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Lakini, kwa kweli, kwa sababu hii nimekuacha uendelee kuwako,+ ili kukuonyesha nguvu zangu na ili nifanye jina langu litangazwe katika dunia yote.+

  • Kumbukumbu la Torati 28:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Na vikundi vyote vya watu wa dunia vitalazimika kuona kwamba jina la Yehova limeitwa juu yako,+ nao kwa kweli watakuogopa wewe.+

  • 1 Wafalme 8:43
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 43 basi na usikilize ukiwa mbinguni, makao yako yaliyofanywa imara,+ nawe ufanye kulingana na yote ambayo mgeni huyo anakuomba;+ kusudi watu wote wa dunia wajue jina lako+ ili wakuogope kama vile watu wako Israeli wanavyokuogopa, na ili wajue kwamba jina lako limeitwa juu ya nyumba hii ambayo nimeijenga.+

  • 1 Wafalme 18:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Na ikawa kwamba wakati+ wa kutolewa kwa toleo la nafaka, Eliya nabii akaanza kukaribia na kusema: “Ee Yehova Mungu wa Abrahamu,+ Isaka+ na Israeli,+ leo na ijulikane kwamba wewe ni Mungu katika Israeli+ na mimi ni mtumishi wako na ni kwa neno+ lako nimefanya mambo haya yote.

  • 2 Wafalme 19:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Na sasa, Ee Yehova Mungu wetu,+ tafadhali, utuokoe+ kutoka mkononi mwake, ili falme zote za dunia zijue kwamba wewe, Ee Yehova, ndiye Mungu peke yako.”+

  • Zaburi 46:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “Salimuni amri, na mjue ya kwamba mimi ni Mungu.+

      Nitatukuzwa kati ya mataifa,+

      Nitatukuzwa duniani.”+

  • Isaya 52:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Yehova ameweka wazi mkono wake mtakatifu mbele ya macho ya mataifa yote;+ na miisho yote ya dunia itauona wokovu wa Mungu wetu.+

  • Danieli 3:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Nami natoa agizo,+ kwamba kikundi chochote cha watu, cha taifa au lugha ambacho kinasema jambo lolote baya juu ya Mungu wa Shadraki, Meshaki na Abednego, kikatwe vipande-vipande,+ na nyumba zao zigeuzwe kuwa choo cha watu wote;+ kwa maana hakuna mungu mwingine yeyote anayeweza kuokoa kama huyu.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki