31 Na ikawa kana kwamba lilikuwa ni jambo dogo zaidi+ kwake kutembea katika dhambi za Yeroboamu+ mwana wa Nebati, sasa akamchukua Yezebeli+ binti ya Ethbaali, mfalme wa Wasidoni,+ kuwa mke wake+ naye akaanza kwenda kumtumikia Baali+ na kumwinamia.
4 Na ikawa kwamba Yezebeli+ alipowakatilia mbali manabii+ wa Yehova, Obadia aliwachukua manabii 100, akawaficha wakiwa vikundi viwili vya watu 50 pangoni, naye akawapa mkate na maji.)+
2 Ndipo Yezebeli akatuma mjumbe kwa Eliya, akisema: “Miungu na ifanye hivyo,+ nayo izidishe jambo hilo,+ ikiwa wakati kama huu hapo kesho sitaifanya nafsi yako iwe kama nafsi ya kila mmoja wao!”
7 Ndipo Yezebeli mke wake akamwambia: “Je, ni wewe unayetawala ukiwa mfalme juu ya Israeli?+ Amka, ule mkate na moyo wako ufurahi. Mimi mwenyewe nitakupa shamba la mizabibu la Nabothi Myezreeli.”+