15 Lakini Yehoyada kuhani akawaamuru wakuu wa mamia, watu waliochaguliwa wa jeshi,+ na kuwaambia: “Mwondoeni katikati ya vikosi, na yeyote atakayemfuata, auawe kwa upanga!”+ Kwa maana kuhani yule alikuwa amesema: “Asiuawe ndani ya nyumba ya Yehova.”
19 Tena akawachukua wakuu wa mamia na walinzi Wakari+ na wakimbiaji+ na watu wote wa nchi, ili wamshushe mfalme kutoka katika nyumba ya Yehova; nao wakaja polepole kupitia njia ya lango+ la wakimbiaji mpaka kwenye nyumba ya mfalme; naye akaanza kuketi juu ya kiti cha wafalme.+