45 “Na laana zote hizo+ hakika zitakujia na kukufuata na kukufikia mpaka utakapokuwa umeangamizwa,+ kwa sababu hukuisikiliza sauti ya Yehova Mungu wako kwa kushika amri zake na kanuni zake alizokuamuru.+
14 Kwa hiyo Hezekia mfalme wa Yuda akatuma ujumbe kwa mfalme wa Ashuru kule Lakishi, na kusema: “Nimetenda dhambi. Rudi nyuma, utoke juu yangu. Lolote utakalonitwika, nitalichukua.”+ Basi mfalme wa Ashuru akaweka juu ya Hezekia mfalme wa Yuda talanta+ 300 za fedha na talanta 30 za dhahabu.
24 Nanyi mnajulishwa kwamba hairuhusiwi kutoza kodi,+ wala ushuru+ wala ada yoyote juu ya yeyote wa makuhani+ na Walawi,+ wanamuziki,+ watunza-milango,+ Wanethini,+ na wafanyakazi wa hii nyumba ya Mungu.