Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 34:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Na Yehova akapita karibu mbele ya uso wake na kutangaza: “Yehova, Yehova, Mungu mwenye rehema+ na neema,+ si mwepesi wa hasira+ naye ni mwingi wa fadhili zenye upendo+ na kweli,+

  • Hesabu 14:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 ‘Yehova, si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi wa fadhili zenye upendo,+ anayesamehe kosa na ubaya,+ lakini ambaye kwa vyovyote hatakosa kuadhibu,+ anayeleta adhabu kwa ajili ya kosa la baba juu ya wana, juu ya kizazi cha tatu na juu ya kizazi cha nne.’+

  • Kumbukumbu la Torati 32:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Kwa maana Yehova atawahukumu watu wake+

      Naye atajuta juu ya watumishi wake,+

      Kwa sababu ataona kwamba tegemeo limetoweka

      Na aliyeko tu ni mtu asiye na uwezo na asiye na thamani.

  • Waamuzi 2:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Na wakati Yehova alipowasimamishia waamuzi,+ Yehova akawa pamoja na mwamuzi huyo, naye akawaokoa kutoka mkononi mwa adui zao siku zote za mwamuzi huyo; kwa maana Yehova alikuwa akijuta+ kwa ajili ya kuugua kwao kwa sababu ya wakandamizaji+ wao na wale waliokuwa wakiwasukuma huku na huku.

  • 2 Samweli 24:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Na malaika+ akaendelea kunyoosha mkono wake kuelekea Yerusalemu ili kuliangamiza; na Yehova akaanza kujuta+ kuhusu msiba ule, na kwa hiyo akamwambia yule malaika aliyekuwa akiwaangamiza watu: “Imetosha! Sasa angusha mkono wako.” Na yule malaika wa Yehova alikuwa karibu na uwanja wa kupuria wa Arauna+ Myebusi.+

  • Zaburi 51:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 51 Ee Mungu, unionyeshe kibali kulingana na fadhili zako zenye upendo.+

      Ufutilie mbali makosa yangu kulingana na wingi wa rehema zako.+

  • Zaburi 69:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Unijibu, Ee Yehova, kwa maana fadhili zako zenye upendo ni njema.+

      Kulingana na wingi wa rehema zako ugeuke kunielekea,+

  • Zaburi 86:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Lakini wewe, Ee Yehova, ni Mungu mwenye rehema na mwenye neema,+

      Si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi wa fadhili zenye upendo na ukweli.+

  • Zaburi 90:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Urudi, Ee Yehova!+ Mpaka wakati gani?+

      Nawe ujute juu ya watumishi wako.+

  • Isaya 63:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Nitazisema fadhili zenye upendo za Yehova,+ sifa za Yehova, kulingana na yote ambayo Yehova ametutendea,+ wema mwingi kwa nyumba ya Israeli+ ambao amewatendea kulingana na rehema+ zake na kulingana na wingi wa fadhili zake zenye upendo.

  • Maombolezo 3:32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Kwa maana, ijapokuwa ameleta huzuni,+ hakika pia ataonyesha rehema kulingana na wingi wa fadhili zake zenye upendo.+

  • Yoeli 2:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Irarueni mioyo yenu,+ wala si mavazi yenu;+ rudini kwa Yehova Mungu wenu, kwa maana yeye ana neema na rehema,+ si mwepesi wa hasira+ naye ni mwingi wa fadhili zenye upendo,+ naye hakika atajuta kwa sababu ya msiba huo.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki