Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 4:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Nanyi mtazishika na kuzifanya, kwa sababu hiyo ni hekima+ kwenu na uelewaji+ kwenu mbele ya macho ya vikundi vya watu watakaosikia juu ya masharti yote haya, nao watasema, ‘Taifa hili kubwa bila shaka ni watu wenye hekima na wenye uelewaji.’+

  • Ayubu 28:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Naye akamwambia mwanadamu,

      ‘Tazama! Kumwogopa Yehova—hiyo ndiyo hekima,+

      Na kuacha ubaya ni uelewaji.’”+

  • Methali 1:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Kumwogopa Yehova ndio mwanzo wa ujuzi.+ Wapumbavu wamedharau hekima na nidhamu.+

  • Methali 9:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Kumwogopa Yehova ndio mwanzo wa hekima,+ na kumjua aliye Mtakatifu Zaidi ni uelewaji.+

  • Mhubiri 12:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Huu ndio mwisho wa mambo, kila jambo limekwisha sikiwa: Mwogope Mungu wa kweli+ na kushika amri zake.+ Kwa maana huo ndio wajibu wote wa mwanadamu.

  • Waebrania 11:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Kwa imani Noa,+ baada ya kupewa onyo la kimungu la mambo ambayo yalikuwa bado hayajaonekana,+ alionyesha woga wa kimungu na kujenga safina+ kwa ajili ya kuiokoa nyumba yake; na kupitia imani hiyo aliuhukumu ulimwengu+ kuwa wenye hatia, naye akawa mrithi wa uadilifu+ unaolingana na imani.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki