28 Na huko mtalazimika kuitumikia miungu mingine,+ kazi ya mikono ya mwanadamu, miti na mawe,+ ambayo haiwezi kuona wala kusikia wala kula wala kunusa.+
17 Lakini mabaki yake huyafanya kuwa mungu, kuwa sanamu yake ya kuchongwa. Huisujudia na kuinama na kuitolea sala na kusema: “Nikomboe, kwa maana wewe ni mungu wangu.”+
26 Pia, mnaona na kusikia jinsi si katika Efeso+ tu, bali pia katika karibu wilaya yote ya Asia, Paulo huyu ameshawishi umati mkubwa na kuwageuza kwenye kauli nyingine, akisema kwamba wale waliofanywa kwa mikono+ si miungu.