24 Kwa mwanadamu hakuna jambo bora kuliko kwamba ale, naam, anywe na kuifanya nafsi yake ione mema kwa sababu ya kazi yake ngumu.+ Hilo pia mimi nimeliona, naam mimi, ya kwamba linatoka kwenye mkono wa Mungu wa kweli.+
22 Nami nimeona kwamba hakuna jambo bora kuliko kwamba mwanadamu afurahie kazi zake,+ kwa maana hilo ndilo fungu lake; kwa kuwa ni nani atakayemleta aone mambo yatakayokuwako baada yake?+
22 Hawatajenga na mtu mwingine akae ndani yake; hawatapanda na mtu mwingine ale. Kwa maana siku za watu wangu zitakuwa kama siku za mti;+ na watu wangu waliochaguliwa wataitumia kazi ya mikono yao wenyewe kikamilifu.+