Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 14:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kwa maana Yehova atamwonyesha Yakobo+ rehema, naye bado hakika atachagua Israeli;+ na kwa kweli atawapa pumziko juu ya udongo wao,+ na mkaaji mgeni ataungana nao, nao watajiunga na nyumba ya Yakobo.+

  • Yeremia 31:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 “Je, Efraimu ni mwana mwenye thamani kwangu, au mtoto anayetendewa kwa upendo?+ Kwa maana kwa kiasi ninachosema vibaya juu yake bila shaka nitamkumbuka zaidi.+ Ndiyo sababu matumbo yangu yamekuwa na msukosuko kwa ajili yake.+ Kwa kuwa nitamhurumia kabisa,”+ asema Yehova.

  • Hosea 1:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Lakini nitaionyesha rehema nyumba ya Yuda,+ nami nitawaokoa kupitia kwa Yehova Mungu wao;+ wala sitawaokoa kwa upinde wala kwa upanga wala kwa vita, wala kwa farasi wala kwa wapanda-farasi.”+

  • Mika 7:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Atatuonyesha rehema tena;+ atayatiisha makosa yetu.+ Nawe utazitupa dhambi zao zote+ katika vilindi vya bahari.

  • Zekaria 10:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Nami nitaifanya nyumba ya Yuda iwe kuu, nami nitaiokoa nyumba ya Yosefu.+ Nami nitawapa makao, kwa maana nitawaonyesha rehema;+ nao watakuwa kama watu ambao sikutupilia mbali;+ kwa maana mimi ni Yehova Mungu wao, nami nitawajibu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki