17 Basi Mungu wa kweli akawapa watoto hao wanne ujuzi na ufahamu katika maandishi na hekima yote;+ naye Danieli alikuwa akielewa maono na ndoto za aina zote.+
23 Nami nakusifu wewe na kukuhimidi,+ Ee Mungu wa mababu zangu, kwa maana umenipa mimi hekima+ na nguvu. Na sasa umenijulisha tulilokuomba, kwa kuwa umetujulisha jambo lile la mfalme.”+
9 “ ‘Ee Belteshaza mkuu wa makuhani wenye kufanya uchawi,+ kwa kuwa mimi mwenyewe najua vema kwamba roho ya miungu mitakatifu imo ndani yako+ na kwamba hakuna siri yoyote ambayo inakusumbua,+ niambie maono ya ndoto yangu ambayo nimeona na tafsiri yake.+