14 Na hakika mtu atauvunja kama vile mtungi mkubwa wa wafinyanzi unavyovunjwa,+ kupondwa vipande-vipande bila mtu kuuachilia, hivi kwamba kati ya vipande vyake vilivyopondwa hakuwezi kupatikana kigae kinachoweza kutumiwa kukusanya moto jikoni wala kuteka maji kutoka eneo lenye matope.”+
28 Je, mtu huyu Konia+ ni umbo tu lililodharauliwa, lililovunjwa vipande-vipande,+ au ni chombo ambacho hakipendezi?+ Kwa nini yeye na uzao wake ni lazima waangushwe chini na kutupwa katika nchi ambayo hawakuijua?’+
38 “‘Juu ya paa zote za Moabu na katika viwanja vyake vya watu wote—vyote—kuna maombolezo;+ kwa maana nimemvunja Moabu kama tu chombo ambacho hakipendezi,’+ asema Yehova.