Hesabu 23:19 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 19 Mungu si mwanadamu kwamba aseme uwongo,+Wala si mwana wa binadamu kwamba ajute.+Je, yeye mwenyewe amelisema naye hatalitenda,Na je, yeye amesema naye hatalitimiza?+ Isaya 55:8 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 8 “Kwa maana mawazo yenu si mawazo yangu,+ wala njia zangu si njia zenu,”+ asema Yehova. Malaki 3:6 Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya 6 “Kwa maana mimi ni Yehova; sikubadilika.+ Nanyi ni wana wa Yakobo; hamjafikia mwisho wenu.+
19 Mungu si mwanadamu kwamba aseme uwongo,+Wala si mwana wa binadamu kwamba ajute.+Je, yeye mwenyewe amelisema naye hatalitenda,Na je, yeye amesema naye hatalitimiza?+