4 Naye hakika atafanya hukumu kati ya mataifa+ na kunyoosha mambo+ kuhusu vikundi vingi vya watu.+ Nao watafua panga zao ziwe majembe na mikuki yao iwe miundu.+ Taifa halitainua upanga juu ya taifa, wala hawatajifunza vita tena.+
9 Na wakaaji wa majiji ya Israeli hakika wataenda na kuteketeza na kuwasha mioto kwa silaha na ngao ndogo na ngao kubwa,—kwa pinde na kwa mishale na kwa fimbo na kwa mikuki; nao watazitumia kuwasha mioto+ kwa miaka saba.
10 Nami nitalikatilia mbali gari la vita kutoka katika Efraimu na farasi kutoka katika Yerusalemu.+ Na upinde wa mapigano+ utakatiliwa mbali. Naye atasema amani kwa mataifa;+ na utawala wake utakuwa kutoka bahari mpaka bahari na kutoka Mto mpaka miisho ya dunia.+