Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 54:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Na wana wako wote+ watakuwa watu waliofundishwa na Yehova,+ na amani ya wana wako itakuwa nyingi.+

  • Yeremia 9:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 “Lakini yule anayejigamba na ajigambe kwa sababu ya jambo hili, kuwa na ufahamu+ na kuwa na ujuzi kunihusu mimi, kwamba mimi ni Yehova,+ Yeye anayeonyesha fadhili zenye upendo, haki na uadilifu duniani;+ kwa maana mimi hupendezwa na mambo hayo,”+ asema Yehova.

  • Yeremia 24:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Nami nitawapa moyo wa kunijua,+ kwamba mimi ni Yehova; nao watakuwa watu wangu,+ nami nitakuwa Mungu wao, kwa maana watarudi kwangu kwa moyo wao wote.+

  • Yeremia 31:34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 34 “Nao hawatafundishana tena kila mtu na mwenzake wala kila mtu na ndugu yake,+ wakisema, ‘Mjueni Yehova!’+ kwa maana wote watanijua mimi, kuanzia yule aliye mdogo zaidi kati yao mpaka yule aliye mkubwa zaidi kati yao,”+ asema Yehova. “Kwa maana nitalisamehe kosa lao, na dhambi yao sitaikumbuka tena.”+

  • Ezekieli 38:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Nami hakika nitajitukuza mwenyewe na kujitakasa mwenyewe+ na kujijulisha mwenyewe mbele ya macho ya mataifa mengi; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’+

  • Waebrania 8:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 “ ‘Nao hawatafundishana kwa vyovyote kila mtu na raia mwenzake wala kila mtu na ndugu yake, wakisema: “Mjue Yehova!”+ Kwa maana wote watanijua mimi,+ kuanzia yule aliye mdogo zaidi mpaka yule aliye mkubwa zaidi kati yao.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki