13 Wamepanda ngano, lakini wamevuna miiba.+ Wamefanya kazi mpaka wakawa wagonjwa; hawatakuwa na faida yoyote.+ Nao hakika wataona aibu kwa ajili ya mazao yenu kwa sababu ya hasira ya Yehova inayowaka.”
11 Basi, kwa sababu mnamtoza mtu wa hali ya chini kodi ya shamba,+ nanyi mnaendelea kuchukua kutoka kwake ushuru wa nafaka; mmejenga nyumba za mawe yaliyochongwa,+ lakini hamtaendelea kukaa ndani yake; nanyi mmepanda mashamba ya mizabibu yenye kupendeza, lakini hamtaendelea kunywa divai yake.+
6 Mmepanda mbegu nyingi, lakini mavuno ni kidogo.+ Mnakula chakula, lakini hamshibi.+ Mnakunywa, lakini hamlewi. Mnavaa nguo, lakini hakuna yeyote anayepata joto; na yeye anayeajiriwa, anaajiriwa kwa ajili ya mfuko wenye matundu.’ ”+