13 Yehova mwenyewe atatokea kama mwanamume mwenye nguvu.+ Ataamsha bidii kama shujaa wa vita.+ Atapaaza sauti, ndiyo, atapiga kelele za vita;+ atajionyesha kuwa mwenye nguvu zaidi juu ya adui zake.+
10 Hawatakuwa na njaa,+ wala kuwa na kiu,+ wala joto kali na jua halitawaunguza.+ Kwa maana Yeye anayewahurumia atawaongoza,+ naye atawaelekeza karibu na mabubujiko ya maji.+
12 Kwa maana hamtaondoka na wasiwasi, wala hamtaenda kwa kukimbia.+ Kwa maana Yehova atakuwa akienda mbele yenu,+ na Mungu wa Israeli atakuwa mlinzi wenu wa nyuma.+
14 Na Yehova mwenyewe ataonekana juu yao,+ na mshale wake utaenda kama umeme.+ Naye Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atapiga baragumu,+ ataenda pamoja na dhoruba za upepo wa kusini.+
5 Nao watakuwa kama wanaume wenye nguvu+ wanaokanyaga matope ya barabarani katika mapigano.+ Nao watajihusisha katika mapigano, kwa maana Yehova yupo pamoja nao;+ na hao wapanda-farasi wataona aibu.+