Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ayubu 31:24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Ikiwa nimeifanya dhahabu kuwa tumaini langu,

      Au nimeiambia dhahabu, ‘Wewe ni tegemeo langu!’+

  • Zaburi 17:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Kwa mkono wako, Ee Yehova, kutoka kwa watu,+

      Kutoka kwa watu wa mfumo huu wa mambo,+ ambao fungu lao liko katika maisha haya,+

      Na ambao tumbo lao wewe hulijaza kwa hazina iliyofichwa,+

      Ambao wametosheka na wana+

      Na ambao huwarundikia watoto wao vitu wanavyoacha.+

  • Zaburi 52:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Huyo ndiye mwanamume ambaye hamweki Mungu kuwa ngome yake,+

      Lakini anategemea wingi wa utajiri wake,+

      Ambaye hulindwa kutokana na shida anazoleta.+

  • Zaburi 62:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Msitegemee upunjaji,+

      Wala kuwa ubatili kwa sababu ya unyang’anyi mtupu.+

      Mali ikiongezeka, msiiweke moyoni.+

  • Yeremia 9:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Yehova amesema hivi: “Mtu mwenye hekima asijigambe kwa sababu ya hekima yake,+ wala mwanamume mwenye nguvu asijigambe kwa sababu ya nguvu zake.+ Mtu tajiri asijigambe kwa sababu ya utajiri wake.”+

  • 1 Timotheo 6:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Uwape maagizo wale walio matajiri+ katika mfumo wa mambo wa sasa wasitake makuu,+ na waweke tumaini lao, si katika utajiri usio hakika,+ bali katika Mungu, ambaye hutupa sisi vitu vyote kwa wingi ili tuvifurahie;+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki