6 Tazama! Nitasimama mbele yako juu ya mwamba huko Horebu. Nawe utaupiga mwamba huo, na maji yatatoka ndani yake, na watu watayanywa.”+ Kisha Musa akafanya hivyo machoni pa wanaume wazee wa Israeli.
8 “Ichukue fimbo+ na kuliita kusanyiko pamoja, wewe na Haruni ndugu yako, nanyi mtauambia mwamba mbele ya macho yao ili kwa kweli utoe maji yake; nawe utawatolea maji kutoka katika mwamba na kuwapa maji kusanyiko na wanyama wao wa kubeba mizigo.”+
14 Yule atakayekunywa maji ambayo nitampa hatapatwa na kiu hata kidogo,+ lakini maji ambayo nitampa yatakuwa chemchemi ya maji+ ndani yake, inayobubujika ili kutokeza uzima wa milele.”+
4 na wote walikunywa maji+ yaleyale ya kiroho. Kwa maana walikuwa wakinywa kutokana na mwamba+ wa kiroho uliowafuata, na mwamba+ huo ulimaanisha Kristo.+