Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 23:40
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 40 Siku ya kwanza, mtachukua matunda ya miti yenu bora, matawi ya mitende,+ matawi ya miti yenye majani mengi na mierebi ya bondeni, nanyi mtashangilia+ mbele za Yehova Mungu wenu kwa siku saba.+

  • Kumbukumbu la Torati 12:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Mtashangilia mbele za Yehova Mungu wenu,+ ninyi na wana wenu, binti zenu, watumwa wenu wa kiume na wa kike, na Mlawi yeyote aliye ndani ya majiji* yenu, kwa sababu hana fungu wala urithi pamoja nanyi.+

  • Kumbukumbu la Torati 12:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Mnapaswa kula vitu hivyo mbele za Yehova Mungu wenu mahali ambapo Yehova Mungu wenu atachagua+—ninyi na wana wenu, mabinti wenu, watumishi wenu wa kiume na vijakazi wenu, na Mlawi yeyote aliye ndani ya majiji* yenu; nanyi mtashangilia mbele za Yehova Mungu wenu katika kazi zenu zote.

  • Kumbukumbu la Torati 14:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Mtakula sehemu ya kumi ya nafaka yenu, divai yenu mpya, mafuta yenu, na wazaliwa wa kwanza wa ng’ombe wenu na kondoo wenu mbele za Yehova Mungu wenu mahali ambapo atachagua jina lake likae hapo,+ ili mjifunze kumwogopa Yehova Mungu wenu sikuzote.+

  • Kumbukumbu la Torati 14:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Kisha mnaweza kutumia pesa hizo kununua chochote mnachotamani, iwe ni ng’ombe, kondoo, mbuzi, divai na vinywaji vingine vyenye kileo, na kitu chochote mpendacho; nanyi mtakula huko mbele za Yehova Mungu wenu na kushangilia, ninyi na familia zenu.+

  • Zaburi 32:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Furahini kwa sababu ya Yehova na kushangilia, enyi waadilifu;

      Pazeni sauti kwa shangwe, ninyi nyote mlio wanyoofu moyoni.

  • Zaburi 100:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Mtumikieni Yehova kwa kushangilia.+

      Njooni mbele zake kwa kelele za shangwe.

  • Wafilipi 4:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Shangilieni sikuzote katika Bwana. Nitasema tena, Shangilieni!+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki