Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kumbukumbu la Torati 4:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Ni lazima mzifuate kwa uangalifu,+ kwa sababu watu watakaosikia kuhusu masharti haya yote wataona kwamba mna hekima+ na uelewaji,+ nao watasema, ‘Kwa hakika watu wa taifa hili kubwa wana hekima na uelewaji.’+

  • Kumbukumbu la Torati 8:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 kumbukeni kwamba Yehova Mungu wenu ndiye anayewapa nguvu za kupata utajiri,+ ili atimize agano lake ambalo aliwaapia mababu zenu, kama ilivyo leo.+

  • Yoshua 1:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 “Ila tu uwe jasiri na imara kabisa, na ufuate kwa uangalifu Sheria yote kama Musa mtumishi wangu alivyokuamuru. Usiende kushoto wala kulia,+ ili utende kwa hekima mahali popote utakapoenda.+ 8 Kitabu hiki cha Sheria kisiondoke kinywani mwako,+ ni lazima ukisome kwa sauti ya chini* mchana na usiku ili ufuate kwa uangalifu mambo yote yaliyoandikwa humo;+ ndipo utakapofanikisha njia yako na kutenda kwa hekima.+

  • 1 Wafalme 2:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Ni lazima utimize wajibu wako kwa Yehova Mungu wako kwa kutembea katika njia zake na kushika maagizo yake, amri zake, sheria zake,* na vikumbusho vyake kama vilivyoandikwa katika Sheria ya Musa;+ ndipo utakapofanikiwa* katika kila jambo unalofanya na kila mahali unapogeuka kwenda.

  • Zaburi 103:17, 18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Lakini upendo mshikamanifu wa Yehova ni wa milele na milele*

      Kuelekea wale wanaomwogopa,+

      Na uadilifu wake kuelekea watoto wa watoto wao,+

      18 Kuelekea wale wanaolishika agano lake+

      Na wale walio waangalifu ili kuyashika maagizo yake.

  • Luka 11:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Lakini Yesu akasema: “Hapana, badala yake, wenye furaha ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika!”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki