-
Hesabu 35:22-24Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
22 “‘Lakini ikiwa alimsukuma au kumtupia kitu chochote na kumuua bila kukusudia au bila chuki na bila nia mbaya,*+ 23 au ikiwa alimwangushia jiwe bila kumwona na mtu huyo akafa, lakini hakuwa adui yake au hakukusudia kumdhuru, 24 basi watu wanapaswa kuhukumu kati ya muuaji na mtu anayelipiza kisasi cha damu, kwa kufuata sheria hizo.+
-
-
Kumbukumbu la Torati 19:4-6Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 “Sasa hivi ndivyo itakavyokuwa kuhusu muuaji ambaye huenda akakimbilia humo ili kuokoa uhai wake: Akimuua jirani yake bila kukusudia naye hakuwa akimchukia;+ 5 kwa mfano, anapoenda na jirani yake msituni kukusanya kuni, kisha anainua mkono wake ili akate mti kwa shoka, lakini shoka lichomoke kwenye mpini na kumgonga jirani yake na kumuua, muuaji huyo anapaswa kukimbilia katika mojawapo ya majiji hayo.+ 6 Asipofanya hivyo, mtu anayelipiza kisasi cha damu+ anaweza kwa hasira kali kumkimbiza, kumkamata, na kumuua, kwa sababu jiji hilo lilikuwa mbali sana. Hata hivyo, hakustahili kufa kwa sababu hakuwa akimchukia jirani yake.+
-