20 Kwa hiyo ikaja kati ya kambi ya Wamisri na kambi ya Waisraeli.+ Upande mmoja, wingu hilo lilikuwa giza. Upande mwingine, uliangaza usiku.+ Hivyo, kambi ya Wamisri haikuikaribia kambi ya Waisraeli usiku kucha.
27 Mara moja Musa akaunyoosha mkono wake juu ya bahari, na asubuhi ilipokuwa ikikaribia, bahari ikarudia hali yake ya kawaida. Wamisri walipokuwa wakiikimbia bahari, Yehova akawakung’uta Wamisri katikati ya bahari.+