Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waamuzi 3:9, 10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Waisraeli walipomlilia Yehova awasaidie,+ Yehova aliwapa mwokozi ili awaokoe,+ Othnieli+ mwana wa Kenasi, ndugu mdogo wa Kalebu. 10 Roho ya Yehova ikamjia,+ akawa mwamuzi wa Israeli. Alipoenda vitani, Yehova alimtia Kushan-rishathaimu mfalme wa Mesopotamia* mikononi mwake, naye akamshinda Kushan-rishathaimu.

  • Waamuzi 11:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Roho ya Yehova ikamjia Yeftha,+ naye akapitia Gileadi na Manase na kufika Mispe kule Gileadi,+ na kutoka Mispe akaenda kupigana na Waamoni.

  • Waamuzi 13:24, 25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 24 Baadaye mwanamke huyo akazaa mwana na kumpa jina Samsoni;+ na mvulana huyo akazidi kukua, na Yehova akaendelea kumbariki. 25 Baada ya muda roho ya Yehova ikaanza kumchochea+ huko Mahane-dani+ kati ya Sora na Eshtaoli.+

  • Waamuzi 14:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Ndipo roho ya Yehova ikamtia nguvu,+ naye akampasua simba huyo vipande viwili, kama mtu anavyompasua mwanambuzi kwa mikono yake. Lakini hakumwambia baba yake au mama yake jambo alilofanya.

  • Waamuzi 15:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Alipofika Lehi, Wafilisti walishangilia sana kumwona. Kisha roho ya Yehova ikamtia nguvu,+ na kamba alizofungwa mikononi zikawa kama nyuzi za kitani zilizochomwa moto, nazo zikalegea* na kuanguka kutoka mikononi mwake.+

  • Zekaria 4:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Ndipo akaniambia: “Hili ndilo neno la Yehova kwa Zerubabeli: ‘“Si kwa jeshi, wala si kwa nguvu,+ bali kwa roho yangu,”+ asema Yehova wa majeshi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki