14 na watu wangu ambao wameitwa kwa jina langu+ wakijinyenyekeza+ na kusali na kuutafuta uso wangu na kuacha njia zao ovu,+ ndipo nitakaposikia kutoka mbinguni na kuwasamehe dhambi yao na kuiponya nchi yao.+
13 Aliendelea kusali kwa Mungu, naye akaguswa na sala yake ya kusihi, akasikia ombi lake la kutaka kibali, akamrudisha Yerusalemu kwenye ufalme wake.+ Ndipo Manase akajua kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli.+
15 Kisha akaondoa katika nyumba ya Yehova+ miungu ya kigeni na ile sanamu iliyochongwa na pia madhabahu zote alizokuwa amejenga kwenye mlima wa nyumba ya Yehova+ na Yerusalemu, akaagiza vitu hivyo vitupwe nje ya jiji.