-
1 Samweli 20:19-22Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 Kufikia siku ya tatu, wataona wazi kwamba haupo, utakuja mahali hapa ulipojificha ile siku nyingine* na ukae hapa karibu na jiwe. 20 Kisha nitapiga mishale mitatu upande mmoja wa jiwe hili kana kwamba ninalenga shabaha fulani. 21 Nitakapomtuma mtumishi, nitasema, ‘Nenda, ukaitafute mishale.’ Nikimwambia mtumishi, ‘Angalia! Mishale iko upande huu wako, ichukue,’ basi unaweza kurudi, kwa maana kwa hakika kama Yehova anavyoishi, hilo linamaanisha kwamba kuna amani katika mambo yako yote na hakuna hatari. 22 Lakini nikimwambia mvulana huyo, ‘Angalia! Mishale iko mbele yako,’ basi ondoka, kwa sababu Yehova anataka uende zako.
-