18 ‘Mimi Yehova, si mwepesi wa hasira, nina upendo mwingi mshikamanifu,*+ ninasamehe makosa na uovu, lakini sikosi kamwe kuwaadhibu wenye hatia, ninawaadhibu wana na wajukuu kufikia kizazi cha tatu na cha nne kwa sababu ya makosa ya baba zao.’+
32 Hata hivyo, Yehonadabu+ mwana wa Shimea,+ ndugu ya Daudi, akasema: “Bwana wangu usifikiri kwamba wamewaua wana wote wa mfalme, kwa maana Amnoni peke yake ndiye aliyekufa.+ Absalomu ndiye aliyeagiza auawe kwa sababu alikuwa amekusudia kufanya hivyo+ tangu Amnoni alipomwaibisha Tamari+ dada yake.+
33 Jambo hilo likamtaabisha mfalme, akapanda kwenye chumba kilicho paani juu ya lango na kulia, alikuwa akisema hivi huku akitembea: “Mwanangu Absalomu, mwanangu, mwanangu Absalomu! Laiti ningekufa badala yako, Absalomu mwanangu, mwanangu!”+