-
2 Samweli 19:41, 42Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
41 Kisha wanaume wote wa Israeli wakaja kwa mfalme na kumuuliza: “Kwa nini ndugu zetu watu wa Yuda walikuiba na kukuleta wewe mfalme na nyumba yako ng’ambo ya Yordani, pamoja na wanaume wako wote?”+ 42 Wanaume wote wa Yuda wakawajibu hivi wanaume wa Israeli: “Kwa sababu mfalme ni mtu wa jamaa yetu.+ Kwa nini jambo hili linawakasirisha? Je, tumekula chochote ambacho kimemgharimu mfalme, au je, tumepewa zawadi?”
-