13 Kisha Yehova akaanza kunguruma mbinguni;+
Aliye Juu Zaidi aliifanya sauti yake isikike+
Kwa mvua ya mawe na makaa ya mawe yanayowaka moto.
14 Alipiga mishale yake akawatawanya;+
Alivurumisha radi yake akawavuruga.+
15 Sakafu za vijito zikaonekana;+
Misingi ya nchi ikafunuliwa kwa kemeo lako, Ee Yehova,
Kwa mlipuko wa pumzi kutoka katika mianzi ya pua yako.+
16 Aliunyoosha mkono wake kutoka juu;
Alinishika na kunivuta kutoka katika maji yenye kina.+