16 Aliunyoosha mkono wake kutoka juu;
Alinishika na kunivuta kutoka katika maji yenye kina.+
17 Aliniokoa kutoka kwa adui yangu mwenye nguvu,+
Kutoka kwa wale wanaonichukia, waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.+
18 Walinikabili katika siku ya msiba wangu,+
Lakini Yehova alikuwa tegemeo langu.
19 Alinitoa nje na kunileta mahali penye usalama;
Aliniokoa kwa sababu alipendezwa nami.+