20 Yehova hunithawabisha kulingana na uadilifu wangu;+
Hunilipa kulingana na usafi wa mikono yangu.+
21 Kwa maana nimezishika njia za Yehova,
Nami sijamwacha kwa uovu Mungu wangu.
22 Hukumu zake zote ziko mbele yangu;
Sitazipuuza sheria zake.
23 Nitabaki bila lawama mbele zake,+
Nami nitajiepusha na uovu.+
24 Yehova na anilipe kulingana na uadilifu wangu,+
Kulingana na usafi wa mikono yangu mbele zake.+