-
1 Wafalme 12:28-30Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
28 Baada ya kushauriana, mfalme akatengeneza ndama wawili wa dhahabu+ na kuwaambia watu: “Inachosha sana kwenu kupanda kwenda Yerusalemu. Ndiye huyu hapa Mungu wenu, enyi Waisraeli, aliyewatoa nchini Misri.”+ 29 Kisha akamweka ndama mmoja kule Betheli,+ na mwingine akamweka kule Dani.+ 30 Na jambo hilo likawafanya watende dhambi,+ watu wakaenda mpaka Dani kuabudu ndama aliyekuwa huko.
-
-
1 Wafalme 13:33, 34Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
33 Hata baada ya mambo hayo kutendeka, Yeroboamu hakuacha njia yake mbaya, lakini aliendelea kuchagua makuhani kutoka miongoni mwa watu wa kawaida ili wahudumu mahali pa juu.+ Alimweka kuwa kuhani* mtu yeyote aliyetaka kuwa kuhani, akisema: “Na awe mmoja wa makuhani wa mahali pa juu.”+ 34 Dhambi hiyo ya nyumba ya Yeroboamu+ ilisababisha waharibiwe na kuangamizwa kutoka duniani.+
-