-
2 Mambo ya Nyakati 23:4-7Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Hivi ndivyo mtakavyofanya: Theluthi moja ya makuhani na ya Walawi watakaoshika zamu+ siku ya Sabato watalinda malango;+ 5 na theluthi nyingine watakuwa katika nyumba ya* mfalme,+ na theluthi nyingine watakuwa katika Lango la Msingi, na watu wote watakuwa katika nyua za nyumba ya Yehova.+ 6 Msimruhusu mtu yeyote aingie katika nyumba ya Yehova isipokuwa makuhani na Walawi wanaohudumu.+ Hao wanaweza kuingia kwa sababu ni kikundi kitakatifu, na watu wote watatimiza wajibu kwa Yehova. 7 Walawi wanapaswa kumzunguka mfalme pande zote, kila mmoja akiwa na silaha zake mikononi mwake. Yeyote atakayeingia katika nyumba hiyo atauawa. Mfuateni mfalme popote aendapo.”*
-