-
2 Mambo ya Nyakati 23:18-21Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Kisha Yehoyada akaweka usimamizi wa nyumba ya Yehova mikononi mwa makuhani na Walawi, ambao Daudi alikuwa amewapanga katika vikundi wahudumu katika nyumba ya Yehova na kutoa dhabihu za kuteketezwa za Yehova+ kulingana na yale yaliyoandikwa katika Sheria ya Musa,+ wakishangilia na kuimba, kama alivyoagiza* Daudi. 19 Aliwaweka pia walinzi wa malango+ karibu na malango ya nyumba ya Yehova, ili mtu yeyote asiye safi kwa njia yoyote ile asiingie. 20 Kisha akawachukua wakuu wa mamia,+ watu mashuhuri, watawala wa watu, na watu wote nchini, wakamsindikiza mfalme kushuka kutoka katika nyumba ya Yehova. Halafu wakaja katika nyumba ya* mfalme kupitia lango la juu na kumweka mfalme kwenye kiti+ cha ufalme.+ 21 Basi watu wote nchini wakashangilia na jiji likatulia, kwa maana walikuwa wamemuua Athalia kwa upanga.
-