-
2 Mambo ya Nyakati 25:17-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Baada ya kushauriana na washauri wake, Mfalme Amazia wa Yuda alituma ujumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu mfalme wa Israeli akisema: “Njoo, tupambane vitani.”*+ 18 Mfalme Yehoashi wa Israeli akatuma ujumbe huu kwa Mfalme Amazia wa Yuda: “Gugu lenye miiba kule Lebanoni lilituma ujumbe huu kwa mwerezi huko Lebanoni, ‘Mpe mwanangu binti yako awe mke wake.’ Hata hivyo, mnyama wa mwituni wa Lebanoni akapita karibu na kulikanyaga-kanyaga gugu hilo lenye miiba. 19 Umesema, ‘Tazama! Nimewaangamiza Waedomu.’+ Kwa hiyo moyo wako umekuwa na kiburi, unataka utukuzwe. Lakini sasa kaa katika nyumba yako mwenyewe.* Kwa nini utafute msiba kisha uanguke, na kuwaangusha pia watu wa Yuda?”
-