-
2 Mambo ya Nyakati 25:25-28Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 Amazia+ mwana wa Yehoashi mfalme wa Yuda aliendelea kuishi kwa miaka 15 baada ya kifo cha Yehoashi+ mwana wa Yehoahazi mfalme wa Israeli.+ 26 Na mambo mengine katika historia ya Amazia, kuanzia mwanzo mpaka mwisho, je, hayajaandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Yuda na wa Israeli? 27 Kuanzia wakati ambapo Amazia aligeuka na kuacha kumfuata Yehova, walipanga njama+ dhidi yake huko Yerusalemu, akakimbilia Lakishi, lakini wakawatuma watu wamfuatie huko Lakishi, nao wakamuua huko. 28 Kwa hiyo wakambeba juu ya farasi na kumrudisha, wakamzika pamoja na mababu zake katika jiji la Yuda.
-