17 Kwa hiyo akamleta mfalme wa Wakaldayo awashambulie,+ ambaye aliwaua wanaume wao vijana kwa upanga+ katika nyumba ya mahali pao patakatifu;+ hakumhurumia kijana wa kiume wala bikira, mzee wala aliye dhaifu.+ Mungu alitia kila kitu mikononi mwake.+
2 “Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Nenda uzungumze na Mfalme Sedekia+ wa Yuda nawe umwambie hivi: “Yehova anasema, ‘Ninalitia jiji hili mikononi mwa mfalme wa Babiloni, naye ataliteketeza kwa moto.+
24Neno la Yehova likanijia tena katika mwaka wa tisa, mwezi wa kumi, siku ya kumi ya mwezi huo, likisema: 2 “Mwana wa binadamu, andika tarehe hii,* siku hiihii ya leo. Mfalme wa Babiloni ameanza kulishambulia Yerusalemu siku hiihii ya leo.+