-
1 Samweli 16:6-10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Walipokuwa wakiingia, Samweli alimwona Eliabu+ na kusema: “Hakika mtiwa-mafuta wa Yehova amesimama hapa mbele zake.” 7 Lakini Yehova akamwambia Samweli: “Usitazame sura yake wala urefu wake,+ kwa maana nimemkataa. Kwa kuwa Mungu haoni kama mwanadamu anavyoona, kwa maana mwanadamu huona kinachoonekana kwa macho, lakini Yehova huona ndani ya moyo.”+ 8 Kisha Yese akamwita Abinadabu,+ akampitisha mbele ya Samweli, lakini Samweli akasema: “Huyu pia Yehova hajamchagua.” 9 Kisha Yese akampitisha Shamma,+ lakini Samweli akasema: “Hata huyu Yehova hajamchagua.” 10 Basi Yese akawapitisha wanawe saba mbele ya Samweli, lakini Samweli akamwambia Yese: “Yehova hajamchagua yeyote kati ya hawa.”
-