-
Yoshua 21:27-33Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
27 Na Wagershoni+ wa koo za Walawi walipewa jiji la makimbilio kwa ajili ya muuaji katika eneo la nusu ya kabila la Manase, yaani, jiji la Golani+ kule Bashani pamoja na malisho yake, na Beeshtera na malisho yake—majiji mawili.
28 Na katika eneo la kabila la Isakari:+ Kishioni na malisho yake, Daberathi+ na malisho yake, 29 Yarmuthi na malisho yake, na En-ganimu na malisho yake—majiji manne.
30 Na katika eneo la kabila la Asheri:+ Mishali na malisho yake, Abdoni na malisho yake, 31 Helkathi+ na malisho yake, na Rehobu+ na malisho yake—majiji manne.
32 Na katika eneo la kabila la Naftali: jiji la makimbilio+ kwa ajili ya muuaji, yaani, jiji la Kedeshi+ kule Galilaya na malisho yake, Hamoth-dori na malisho yake, na Kartani na malisho yake—majiji matatu.
33 Wagershoni walipewa jumla ya majiji 13 na malisho yake kulingana na koo zao.
-