Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Samweli 6:3-8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Hata hivyo, wakaweka Sanduku la Mungu wa kweli juu ya gari jipya la kukokotwa+ ili walisafirishe kutoka katika nyumba ya Abinadabu,+ iliyokuwa kwenye kilima; na Uza na Ahio, wana wa Abinadabu, walikuwa wakiliongoza gari hilo jipya.

      4 Basi wakalisafirisha Sanduku la Mungu wa kweli kutoka katika nyumba ya Abinadabu iliyokuwa kwenye kilima, na Ahio alikuwa akitembea mbele ya Sanduku hilo. 5 Daudi na nyumba yote ya Israeli walikuwa wakisherehekea mbele za Yehova kwa ala za kila aina zilizotengenezwa kwa mbao za mberoshi, vinubi, vinanda vinginevyo,+ matari,+ matasa, na matoazi.+ 6 Lakini walipofika kwenye uwanja wa kupuria wa Nakoni, Uza akaunyoosha mkono wake haraka na kulikamata Sanduku la Mungu wa kweli,+ kwa sababu ng’ombe walikuwa karibu kuliangusha. 7 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Uza, na Mungu wa kweli akamuua+ papo hapo kwa sababu ya tendo lake lisilo la heshima,+ akafa hapo karibu na Sanduku la Mungu wa kweli. 8 Lakini Daudi akakasirika kwa sababu hasira kali ya Yehova iliwaka dhidi ya Uza; na tangu siku hiyo mahali hapo panaitwa Peres-uza.*

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki