-
2 Samweli 6:3-8Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Hata hivyo, wakaweka Sanduku la Mungu wa kweli juu ya gari jipya la kukokotwa+ ili walisafirishe kutoka katika nyumba ya Abinadabu,+ iliyokuwa kwenye kilima; na Uza na Ahio, wana wa Abinadabu, walikuwa wakiliongoza gari hilo jipya.
4 Basi wakalisafirisha Sanduku la Mungu wa kweli kutoka katika nyumba ya Abinadabu iliyokuwa kwenye kilima, na Ahio alikuwa akitembea mbele ya Sanduku hilo. 5 Daudi na nyumba yote ya Israeli walikuwa wakisherehekea mbele za Yehova kwa ala za kila aina zilizotengenezwa kwa mbao za mberoshi, vinubi, vinanda vinginevyo,+ matari,+ matasa, na matoazi.+ 6 Lakini walipofika kwenye uwanja wa kupuria wa Nakoni, Uza akaunyoosha mkono wake haraka na kulikamata Sanduku la Mungu wa kweli,+ kwa sababu ng’ombe walikuwa karibu kuliangusha. 7 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya Uza, na Mungu wa kweli akamuua+ papo hapo kwa sababu ya tendo lake lisilo la heshima,+ akafa hapo karibu na Sanduku la Mungu wa kweli. 8 Lakini Daudi akakasirika kwa sababu hasira kali ya Yehova iliwaka dhidi ya Uza; na tangu siku hiyo mahali hapo panaitwa Peres-uza.*
-