-
2 Samweli 5:19-21Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 Daudi akamuuliza Yehova:+ “Je, nipande kwenda kuwashambulia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Ndipo Yehova akamwambia Daudi: “Panda uende, nami hakika nitawatia Wafilisti mikononi mwako.”+ 20 Basi Daudi akaenda Baal-perasimu na kuwaua huko. Ndipo akasema: “Yehova amewapasua na kuwapita+ maadui wangu mbele yangu, kama ufa uliopasuliwa na maji.” Ndiyo sababu alipaita mahali hapo Baal-perasimu.*+ 21 Wafilisti wakaacha sanamu zao hapo, na Daudi na wanaume wake wakazichukua na kwenda nazo.
-